Kocha mfaransa wa Simba Pierre Lechatre amebakiza siku 43 kwenye mkataba wake wa kuifundisha Simba. Mkataba wa Lechatre utamalizika June ...

Lechatre abakiza siku 43 tuu kumaliza mkataba na Simba SC


Kocha mfaransa wa Simba Pierre Lechatre amebakiza siku 43 kwenye mkataba wake wa kuifundisha Simba.

Mkataba wa Lechatre utamalizika June 18, 2018 ambapo atakuwa huru kuondoka au kubaki Simba kama watahitaji kuendelea nae.

Haji Manara akiwa Kenya amethibitisha kwamba mkataba wa kocha wao unaelekea ukingoni na amewaomba wanasimba kuwa watulivu na wavumilivu wakisubiri uongozi uamue kama utaendelea au utaachana na kocha huyo.

“Kocha Lechantre mkataba wake unamalizika mwezi June 18, 2018 uongozi utakaa nae utaona kama ipo haja ya kuendelea nae au la”-Haji Manara.

Lechantre alisaini mkataba wa kuifundisha Simba katikati ya msimu akichukua nafasi ya Joseph Omog ambaye alitimuliwa.

0 comments:

ONLINE USERS