Baada ya tetesi kwamba Deus Kaseke huenda akaungana na kocha Hans van Pluijm pamoja na Tafadzwa Kutinyu kutoka Singida United kujiunga Az...
Kaseke wa Singida United apata mchongo Sauz
Baada ya tetesi kwamba Deus Kaseke huenda akaungana na kocha Hans van Pluijm pamoja na Tafadzwa Kutinyu kutoka Singida United kujiunga Azam, mkurugenzi wa Singida United amesema Kaseke atatimkia South Afrika ambako amepata ofa.
Festo Sanga amekanusha taarifa za muda mrefu ambazo zimekuwa zikimhusisha Kaseke kujiunga na Azam kutokana na uhusiano wake mzuri na Hans van Pluijm ambaye ametangazwa kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo.
“Deus Kaseke amepata ofa kutoka South Afrika, kuna timu imepanda ligi kuu ya huko inamuhitaji Kaseke. Sina taarifa kwamba anakwenda kuungana na kocha Hans”-Festo Sanga.
Kaseke alijiunga na Yanga wakati Pluijm akiwa kocha mkuu wa ‘timu ya wananchi’ wawili hao wakaungana tena Singida United inawezekana ndiyo sababu ya kuhusishwa tena kutaka kufanya kazi pamoja Azam FC.
About author: Udaku
Cress arugula peanut tigernut wattle seed kombu parsnip. Lotus root mung bean arugula tigernut horseradish endive yarrow gourd. Radicchio cress avocado garlic quandong collard greens.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: